1. Isa 9:1-4
|
2.1Kor
1:10-13,17
|
Injili: Mt 4:12-23
|
" Ili kupata samaki wazuri
uvumilivu wahitajika"
Wapendwa
katika Kristu, leo tunaadhimisha jumapili ya tatu ya kipindi cha kawaida cha
mwaka ambapo katika masomo yetu hasa somo la Injili tunasikia Yesu anawaita
wafuasi wake wa kwanza kabisa: Peter,
Andrea, Yakobo na Yohane ( Mt4:12-23). Hawa walioitwa kumfuata Kristu kazi yao
kabla ya hapo ilikuwa ni kuvua samaki, lakini tunaona leo Yesu anawaita wawe
wafuasi wake ili wawe ni wavuvi wa watu. Hawa ni kundi la watu ambao walikuwa
na mtizamo na fikra za aina fulani katika maisha yao, lakini Kristu anatumia
hiyo fursa ya huo mtizamo wao kuwa fursa yenye mtizamo zaidi ya ule mtizamo
waliokuwa nao wale wavuvi wa samaki, huo mtizamo wa Bwana wetu Yesu Kristu kwa
wale aliowaita wawe wafuasi na wanafunzi wake, ni mtizamo wa kutoka na kuingia
ndani zaidi kwenye maisha ya watu baadala ya maisha ya viumbe vingine.
Ndugu
wapendwa katika Kristu tunapata kujifunza kuwa Kristu anvyowaita hawa wafuasi
wake wa kwanza kuacha kazi ya uvuvi na kumfuata ili wawe wavuvi wa watu,
tunapata fundisho kuwa ziwa/ bahari daima kadiri ya tafsri ya maandiko
matakatifu ni ishara ya uovu/ubaya, hivyo Kristu anavyowaambia kuwa waende duniani
wakawavue watu, anagusia dhana ya watu waovu, na maovu yao duniani. Dunia
tunayoishi imejaa mema na maovu pia, hii dunia yaweza pia chukua picha/taswira
ya ziwa au bahari ambapo ziwani au baharini kuna aina mbalimbali za viumbe,
wakiwemo samaki wa aina mbalimbali. Ni katika mtizamo huu tunaona Yesu anawaita
hawa waende katika ile bahari kubwa sana ili waweze kuwavua watu, kwa maana ya
kuwafundisha watu fadhila za Krikristu kutoka fadhila za kidunia.
Swali
ambalo twaweza jiuliza na pia likapata kutuongoza katika tafakari yetu ni
kwamba kwa nini Yesu anawaita hawa wavuvi? twaweza jibu hili swali
tukiambatanisha sifa alizo nazo mvua samaki. Kwa msingi huu hizi ndoo sifa
ambazo anazo mvua samaki Kristu anazitumia katika kutufikishia ujumbe wa Neno
la Mungu. Hebu tuone hizo sifa:
Kwanza,
mvua samaki ni mtu ambaye ana uvumilivu wa hali ya juu. Daima mvua samaki huwa
na uvumilivu katika kufanya kazi yake ya kuvua akirusha ndoana au jalife bahari
au ziwani au mtoni huwa anakuwa na subira hadi kuhakikisha kuwa samaki
wanaingia katika hilo jalife. Ni kwa msingi huu twaweza baini kuwa katika
kuwahubiri Neno la Mungu wale ambao bado hawajaipata habari njema ya wokovu,
daima kunahitaji uvumilivu, maana watu hawawezi wakabadilishwa na mahubiri au
tafakari ya siku moja, hivyo ni lazima na muhimu kuwa na uvumilivu katika
kutangaza habari njema ya Bwana. Walisikialo neno la Bwana hupata kuelewa Neno,
na kubadilika kufuatana na uvumilivu wa mchungaji.
Pili,
mvua samaki daima huwa na ile sifa ya kutokata tamaa. Daima mvuvi akirusha
ndoana baharini, hasipofanikiwa hurudia tena na tena hadi kuhakikisha kuwa
anafanikiwa, hivyo kwetu ni fundisho kuwa katika maisha yetu ya Kikristu
hatuhitaji kukata tamaa pale ambapo tunaona maisha yetu ya utume, maisha yetu
kama wakristu hayaendi, au pale ambapo tunaona giza katika maisha ya ufuasi wa
Bwana wetu Yesu Kristu, daima kwa neema
ya Mungu tunahitaji tuwe imara na tuwe na ile roho ya kutokata tamaa.
Tatu,
mvua samaki huwa na ile sifa ya kuwa shupavu. Mvua samaki daima huwa yupo
tayari kukumbana na mawimbi makali ya bahari au ziwa au mto, huwa tayari kuweka
maisha yake mdomoni mwa wanyama wakali wa bahari kama vile Mamba, Nyangumi,
viboko, nk hayo yote huyapitia ili aweze kupata anachohitaji kupata katika
safari yake. Vile vile wahubiri, wachungaji daima hupata changamoto katika
bahari ya maisha. Daima huwa ni changamoto kuwahubiria watu ukweli na wote
wakaukubali ukweli. Hivyo daima ni dhahiri kuwa katika kuhubiri ukweli lazima
yule atangazaye Neno la Mungu hupata changamoto za kutukanwa, au kukataliwa kwa
sababu ya kusimamia ukweli wa Neno la Mungu. Yule ahubiriye ukweli ndoo yule
atakaye chukiwa na ndugu zake, atakayetemewa mate na saa nyingine atakeye
tukanwa na watu, yule asimamaye katika njia ya haki na ukweli daima huwa na
marafiki wachache. Katika hili tunaalikwa kuuishi kuhubiri na kuishi ukweli.
Nne,
mvuvi daima huwa ana akili ya kusoma alama za nyakati katika kutenda kazi
yake. Mvua samaki hujua kuwa haya ni
majira ya kupata samaki wengi, na pengine hujua na kutabiri kuwa muda fulani
siyo rahisi kuwapata samaki. Anajua ni lini arushe jarife baharini, au aweke
ndoana baharini. Mvuvi anajua tosha kuwa siyo kila majira samaki wana patikana
kwa wingi, bali yeye hujua majira ya kuwapata samaki wengi na majira ambapo
samaki huwa daima ni wachache au saa nyingine hakuna kabisa. Hivyo katika
kutangaza Neno la Bwana hatuna budi kusoma alama za nyakati na kutambua kuwa
huu ni wakati wa watu kuukubali ujumbe wa Neno la Mungu, au hu ni wakati watu
kutokubali kiurahisi Neno la Mungu. Ni kwa msingi huu twaweza baini muda wa
kusikiliza{ kutafakri} na muda wa kuongea na watu.
Tano,
mvuvi mwerevu huwa na anajua namna ya kutupa chambo baharini au ziwani ili
apate kumpata samaki vyema. Mhubiri mzuri ni yule anayetambua kuwa hawezi kuwavuta watu wote kwake, mtangaza Neno la
Mungu, daima anahitaji kujua mazuri yake na mapungufu yake. Hivyo katika
kutangaza Neno la Bwana daima tutambue kuwa kuna nyakati ambazo kile
tukihubilicho kinaendana na maisha yetu wenyewe, na pia maisha ya watu
tuwahubilio.
Mwisho,
mvuvi mwerevu daima huwa anajitahidi kuficha kivuli chake pindi avuapo samaki,
maana hasipoficha hicho kivuli hatofanikiwa kupata hata samaki mmoja. Vivyo
hivyo muhubir mzuri na mwerevu hawahubiri au hatangazi Neno la Bwana kufuatana
na hisia na vionjo vyake, bali muhubiri mwema na mzuri huwahubiria watu maisha Kristu. Mhubiri mwema
daima huvaa utu na sura Kristu. Mhubiri ni Kristu mwingine katika kuwafanya
watu walielewe neno la Mungu. Lengo la mhubiri daima ni kuwafanya watu waweke
macho na mioyo yao kwa Kristu kuliko kuwafanya watu wahamishie mioyo na macho
yao kwake ( kuishi maisha yenye kupendeza, maisha yenye kumbeba na kumpeleka
Kristu kwa wengine).
Ndugu
wapendendwa twaweza tambua kuwa kila mmoja wetu ameitwa na Bwana katika
kumtumikia, hivyo ni mwaliko kwetu sote kutumia kalama zetu, na mapaji yetu
tuliyojaliwa na Mungu katika kuhubiri Neno la Bwana. Kila mmoja anaitwa na
Kristu na kutumwa na Kristu kuwa mmisionary pale alipo. Lile lolote ambalo kila
mmoja wetu afanyalo alifanye kwa utukufu wa Bwana kwani ni huyo Bwana ambaye
hutoa kwa kila mmoja wetu kadiri ya mapenzi yake.
No comments:
Post a Comment